Home

HOME I

Tuesday, November 9, 2010

Relief From Headache In Natural Ways

                                                         
Headache is a common problem, specially among the working crowd. Headache is caused due to several factors, but we can put it under three broad categories -

1.Tension – This is the most common cause of headache. Tension creates a spasm of the muscles at the back of the neck. The muscle spasm gets the tissues over the surface of the cranium and thus, the pain is felt not only on in the neck but also on the forehead.

2.Migraine – Migraine is the abnormality of the nervous system. This strain on the nervous system is caused due to eye strain, shock, stomach disorders etc. Migraine is a chronic disease which needs medical attention.

3.Cluster Headache – Cluster headaches are repetitive and gets back several times in a month. These are generally caused due to constant pressure on the nerves like alcohol consumption, chain smoking etc.

Headaches are very disturbing and restricts your attention to the pain alone. At this moment pain killer seems to be the only solution to get relief form headache. Pain killers, however, have side effects. Here are few home remedies to get relief from headache -

1.For chronic headache, eat sliced apple with salt everyday in the morning for a week.

2.Crush lemon crust into a fine powder and make it into a paste with the use of water. Apply this on the forehead. This is quick relief form headache caused due to tension.

3.Apply a small amount of Eucalyptus oil on the center of the head and cover it with a towel dipped in warm water. This is one of the most effective ways of curing pain.

4.Put 3 drops of ghee in your nostrils for a week to get rid of headache from cold.

5.Drink a glass of water with a teaspoon of honey every morning to treat chronic headache.

6.Grind watermelon seeds with poppy seeds and consume three grams of it everyday if you are suffering constant pain.

7.Application of sandalwood paste on the forehead is one of the tradition ways of curing headache.

These seven tips will surely give you quick relief from headache and does not have any side effects. They not only get you relief from headache but also treats it, so that you don't suffer the symptoms again.

Sunday, November 7, 2010

mnara wa kuongozea meli feri waleta taswira nzuri

Mashoga Ruksa kuwa Wanajeshi Marekani

JESHI la Marekani limekubali kuanza kutoa mafunzo ya kijeshi kwa mashoga baada ya wiki iliyopita Jaji wa Jimbo la California kutengua sera ya 'usiulize, usimwambie'. Sera hiyo ilikuwa ikipinga wazi mashoga kutumikia jeshi ingawa Wizara ya Ulinzi imewaonya wanajeshi mashoga ikisema kuwa huenda sheria hiyo ikatenguliwa.

Habari kutoka mjini Washington DC zimeeleza kuwa, pamoja na sera hiyo ya kupinga mashoga kutumikia jeshi kutenguliwa, Pentagon imekata rufaa kuhusu uamuzi huo na kumtaka Jaji kurejesha kwa muda sera hiyo lakini Jaji Virginia Phillips jana alikataa ombi hilo.

Imeelezwa kuwa baada ya kuondolewa sera hiyo, makundi ya wanaharakati wa kutetea haki za mashoga wamepanga kupeleka watu wa jamii hiyo kwenye vituo vya mafunzo ya kijeshi ili kujaribu tamko hilo la Pentagon.

"Endapo wenyewe binafsi watakubali wazi kuwa ni mashoga na wanataka kujifunza jeshi, tutawafanyia utaratibu lakini tutawaeleza kuwa hali hiyo kisheria inaweza kubadilika," amesema msemaji wa Idara ya Mafunzo ya Kijeshi katika kituo cha Fort Knox, Kentucky, Douglas Smith.

Mwezi Septemba mwaka huu, Chama cha Democrats kilijaribu kuitengua sera hiyo ya kuzuia mashoga kutumikia jesheni kupitia Baraza la Seneti lakini kikashindwa baada ya kushindwa kupata kura za kutosha.

Naye Rais Barack Obama, alishatangaza kuiondoa sera hiyo lakini wengi wa washauri wake wanakubali kuwa Rais huyo hawezi kuondoa sera hiyo ya kuwapiga marufuku mashoga kutumikia wazi jeshini bila kupitishwa na Baraza la Congress ama hatua za kisheria.

Katika hatua nyingine, Pentagon imesema kuwa Desemba mosi mwaka huu, inatarajia kutoa taarifa kuhusu uwezekano wa kuwepo madhara watakapowaruhusu wazi mashoga kutumikia jeshini.

Baadhi ya maofisa wa Pentagon wanasema kuwa kuwaruhusu mashoga kutaleta mabadiliko ya kila kitu jeshini kuanzia nyumba, bima na itifaki katika shughuli za kijamii.

Mjini California, Jaji Phillips anadai kuwa sera hizo zinavuruga haki za wanajeshi mashoga kuwa huru kuzungumza na kupata ulinzi sawa chini ya sheria.

Kesi ya kupinga kuzuiwa mashoga jeshini ilifunguliwa na kundi kutoka chama cha Republicans kinachounga mkono mashoga kwa niaba ya wanajeshi mashoga ambao walitimuliwa.


                                            Source: DarLeo

Ni kichuma kidogo Lakini chatingishwa watu duniani

Muslims dismissive of Obama's visit in India

                                                                        
Muslims from across India have downplayed the hype surrounding US President Barack Obama's visit this week, saying they did not expect him to do anything to improve the condition of Muslims in India or abroad. Members of the minority community in India that constitute roughly 12 percent of its 1.2 billion people, said Obama had said and promised much, but delivered little, during his two years in office.

                        

KIKWETE AAPISHWA KUWA RAISI

                   Raisi mteule Jakaya Mrisho Kikwete akiapa kwa kushika kitabu kitakatifu (TheHolly Qur'an ) mbele ya Jaji mkuu wa Tanzania Jaji  Agustino Ramadhani.


Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ameapishwa baada ya kushinda matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31, 2010.

Rais ameapa mbele ya jopo la viongozi wa serikali wakiwemo Jaji Mkuu, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Katibu Mkuu Kiongozi, Jopo  la Majaji, Wakuu wa Vyombo vya ulinzi, Viongozi Watatu wa Madhehebu ya Dini, Wazee Wawili kutoka Tanzania Bara na Tanzania Visiwani  na Karani wa Baraza la Mawaziri.


Jakaya Kikwet, akiwasili uwanjani katika gari la wazi akiwasili kwa ajili ya kuapishwa

                                         















KIKWETE ASHINDA URAISI KWA 61.7%



                                                                      
                                   
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)  ilimtangaza Kikwete aliyekuwa akigombea nafasi hiyo kwa tiketi ya CCM, kuwa mshindi baada ya kupata kura 5,276,827 (sawa na  61.17%) ya kura zote halali zilizopigwa 8,626,283.

Akitangaza matokeo hayo Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Lewis Makame, alisema Kikwete alipata ushindi huo, miongoni mwa wagombea wa vyama saba vya siasa waliowania.

Aliyekuwa mgombea wa Chadema, Dk Willibrod Slaa hakuhudhuria hafla hiyo kutokana na kile alichodai juzi kuwa hakubaliani na matokeo.

Kwa mujibu wa matokeo hayo, nafasi ya pili katika kinyang’anyiro hicho ilichukuliwa na Willibrod Slaa wa Chadema ambaye alipata kura 2,271,941 (sawa na 26.34%) ya kura zote halali.

Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF, alishika nafasi ya tatu kwa kupata kura 695,667 (sawa na  8.06% ) ya kura zote halali.

Baada ya kutangaza matokeo hayo, Rais Kikwete aliwashukuru wapiga kura, NEC na vyombo vya habari kwa kuwezesha uchaguzi huo kufanyika kwa utulivu na amani.

Alisema, “ushindi niliopata unaonesha imani ya wapiga kura kwangu na ninaahidi nitawatumikia kwa ari mpya zaidi, nguvu mpya zaidi na kasi mpya zaidi.” .

Thursday, November 4, 2010

Dr Slaa : Matokeo yamechakachuliwa...

 











                          



   Dk Willibrod Slaa.
MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa jana alitoa tuhuma nzito dhidi ya Idara ya Usalama wa Taifa akisema kuwa taasisi hiyo imemuibia kura na hivyo hatayakubali matokeo ya uchaguzi wa urais.

Kauli hiyo imetolewa wakati Tume ya Uchaguzi (Nec) ikielekea kukamilisha kutangaza matokeo ya majimbo na kumtangaza mshindi, jambo ambalo litamfanya Dk Slaa na chama chake kuzuiwa na katiba ya nchi kupinga matokeo hayo mahakamani.

Dk Slaa aliwaambia waandishi wa habari jana akisema kuwa: "Kuna uchakachuaji mkubwa wa kura na kazi hiyo inafanywa na Usalama wa Taifa," alisema Dk Slaa ambaye matokeo yanayotangazwa na Nec yanaonyesha kuwa anaendelea kushika nafasi ya pili akiwa nyuma ya mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete.

Lakini Mwenyekiti wa Nec, Jaji Lewis Makame alipoulizwa kuhusu tamko hilo la Chadema, alimtaka Dk Slaa kuwasilisha taarifa zinazothibitisha madai aliyoyatoa kuwa Nec imekuwa ikitangaza matokeo yaliyochakachuliwa tofauti na zile alizopata.

Jaji Makame alisema kama madai ya Dk Slaa ni ya kweli, ni muhimu apeleke hizo idadi ya kura alizodai amepunjwa ili kuthibitisha madai yake dhidi ya tume hiyo.

Alisema idadi ya kura zinazotangazwa na Nec kwenye kinyang’anyiro cha urais ni zile ambazo wagombea hao wamezipata kihalali kwenye upigaji kura na wala hakuna upendeleo wowote.

“Mimi sijapata malalamiko yoyote kutoka kwa mgombea huyo, hivyo kama anayoyazungumza ni ya kweli kuna umuhimu wa kuthibitisha hiyo tofautu anayodai ipo, lakini kura tunazotangaza ni kura ambazo kila mgombea alizipata kwenye uchaguzi," alisema Jaji Makame
Mbunge huyo wa zamani wa Jimbo la Karatu alionya kama Nec inaitakia mema nchi hii, ifute matokeo yote ya urais na uchaguzi urudiwe upya.

"Hatuwezi kukubali matokeo yanayopikwa na Usalama wa Taifa. Hayo si matakwa ya wananchi," alisema Dk Slaa baadaye kukaririwa kwenye TBC.

Kwa mujibu wa Dk Slaa, ambaye pia ni katibu mkuu wa Chadema, chama chake kimekuwa kikifuatilia kwa makini matokeo hayo na kugundua wizi mkubwa wa kura kwenye nafasi za urais na ubunge.

Mgombea huyo wa urais, ambaye mara nyingi hujenga hoja kwa kutumia ushahidi, alisema moja ya maeneo waliyogundua kuwepo kwa wizi wa kura ni matokeo ya Jimbo la Geita lililo mkoani Mwanza ambako alidai Nec ilitangaza kuwa kwenye uchaguzi wa rais, CCM imepata kura 17,792 na Chadema kura 3,789.

Lakini akasema kwa mujibu wa fomu walizonazo ambazo zilisainiwa na mawakala wao kwenye kata 20 za jimbo hilo, CCM ilipata kura 30,960 na Chadema 15,736.

"Nashangaa Nec wanatangaza matokeo haya kutoka wapi? Hayo ya Geita ni moja tu. Kule Hai, fomu zinaonyesha kwenye urais CCM ina kura 20,120 na Chadema 26,724, lakini Nec imetangaza kuwa CCM ina kura 35,910 na Chadema kura 18,513," alisema Dk Slaa huku akionyesha baadhi ya fomu kwa waandishi wa habari.

Dk Slaa pia alitoa mfano aliodai kuwa wizi wa kura katika kituo namba 00070103 cha Ubungo jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa fomu 24A inaonyesha CCM wamepata kura 68,727 na Chadema 65,450, lakini matokeo ya kata za Ubungo yanaonyesha CCM ina kura 70,472 na Chadema 72,252.

Dk Slaa alisema mbali na Ubungo, tatizo hilo pia alidai liko Kigoma Mjini ambako Chadema imeshinda kwa zaidi ya kura 500, lakini "matokeo yalichakachuliwa na kusababisha vurugu hadi askari wakawapiga mabomu wafuasi wa Chadema".

Pia alisema kwenye Jimbo la Segerea, ambako matokeo yalicheleweshwa kwa siku mbili na kutangazwa usiku wa manane juzi, mambo ni mabaya zaidi kwa kuwa fomu 21 A na B hazikuwepo na wasimamizi walikwenda nazo majumbani kulala.

"Kiwalani fomu hazikuwepo na matokeo hayakuonekana. Kipawa vituo vinne matokeo hayakuonekana na Vingunguti kuna vituo saba na Tabata vituo viwili ambako matokeo hayakuonekana," alisema Dk Slaa.

Aliongeza kusema: "Hali kama hiyo pia imetokea Morogoro Mjini. Matokeo hayajaonekana na yametangazwa tu. Kibakwe na Kiteto mgombea hakushirikishwa katika kutangaza matokeo.

"Hayo ni majimbo ya mifano tu. Yapo majimbo mengi na kutokana na hali hiyo, Chadema imetoa tahadhari kwa Tume na vyombo vya ulinzi na usalama kuwa taratibu hazijafuatwa na nyingi zimevunjwa."

Dk Slaa alisema kuwa ni muhimu waangalizi wote wa uchaguzi wakatoa taarifa zao hadharani ili kusaidia nchi na kumtaka mkuu wa Jeshi la Polisi kuendesha chombo hicho cha dola kwa haki na maadili waliyosaini.
Baadaye mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kuwa kauli hiyo ya Dk Slaa ni tamko rasmi la Chadema.

Akizunguzia ucheleweshaji wa mataokeo unaodaiwa kutokea kwenye majimbo ambayo CCM imeonekana kukabwa koo na vyama vyama vya upinzini, Jaji Makame alisema wao wanatangaza matokea wanayopelekewa na wala hakuna ucheleweshaji wowote.

Mkuu wa kitengo cha uchaguzi cha CCM, Mattson Chizi alisema hoja za Dk Slaa zimejikita kwenye matokeo yanayotangazwa na Nec hivyo hawezi kuzungumzia suala hilo.
"Tunachosubiria ni matokeo ya jumla na hatuwezi kuingilia kazi ya tume," alisema.

Kwa upande wa CUF, Meneja wa Kampeni wa chama hicho, Said Miraji, alisema aligoma kuzungumzia suala akieleza kwamba CUF kitaandaa taarifa kuhusu uchaguzi ambayo itatolewa baadaye na mgombea urais wao, Prof Ibrahim Lipumba.


CHANZO: MWANANCHI

Tuesday, November 2, 2010

MR II a.k.a SUGU ASHINDA UBUNGE MBEYA MJINI

Msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Joseph Mbilinyi aka MR II (Sugu ) ameshinda uchaguzi wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya CHADEMA kwa kumbwaga vibaya mgombea wa CCM na wagombea wengine.


MR II alishinda uchaguzi wa Mbeya Mjini kwa kuwabwaga vibaya wapinzani wake, Benson Mpesya wa CCM, Prince Mwaihojo, wa CUF, Tokolasi Kasuluari wa DP na Aggabo Mwakatobe wa NCCR.

Msimamizi wa jimbo hilo alimtangaza MR II kuwa ni mshindi wa jimbo hilo baada ya kupata kura 46,411 huku mpinzani wake mkubwa toka CCM, Benson Mpesya akifuatia kwa mbali akiwa na kura 24,327.